Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Hakimiliki Tanzania

To protect the rights of content creators...
SHULE YA SEKONDARI MAKONGO YASHIRIKI MASHINDANO YA KIMATAIFA YA MILIKI UBUNIFU ZIMBABWE
13 Aug, 2026
SHULE YA SEKONDARI MAKONGO YASHIRIKI MASHINDANO YA KIMATAIFA YA MILIKI UBUNIFU ZIMBABWE

Shule ya Sekondari Makongo yashiriki mashindano ya Kimataifa ya Miliki Bunifu yaliyofanyika nchini Zimbabwe tarehe 29 Mei, 2026  mashindano hayo yaliratibiwa na Ofisi ya Hakimiliki Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Miliki Bunifu la Kikanda la Afrika (ARIPO) .

Mashindano hayo yamelenga kutoa elimu ya miliki bunifu mashuleni na kukuza vipaji vya ubunifu kwa Wanafunzi wa Shule za Sekondari.

Kitaifa mashindano hayo yalihusisha Shule tano ambazo zilikuwa ni Shule ya Ufundi Tanga, Shule ya Sekondari Sikirari, Shule ya Sekondari Kiembe Samaki - Zanzibar, St. Joseph Sekondari na Makongo Sekondari  waliibuka washindi  kitaifa. 

Kimataifa mashindano hayo yamehusisha Wanafunzi kutoka nchi tano za Afrika ikiwemo Gambia,Ghana,Zambia,Liberia na Rwanda.
 

slot gacor