Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akimwapisha Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Paul Makonda (Mb) Leo tarehe 13 Januari, 2026 katika Ikulu ya Chamwino Jijini Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Hamis Mwinjuma kuwa Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo leo Novemba 18, 2025 Ikulu jijini Dodoma.
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu na Msimamizi wa Hakimiliki COSOTA Bw. Philemon Kilaka (wapili kushoto) akikabidhi leseni kwa mwanzilishi wa Kampuni ya Society of Music Advocacy Limited (SOMA), Bw. Fareed Kubanda (wapili kulia) itakayofanya jukumu la kukusanya na kugawa mirabaha kwa kazi za muziki tarehe 23 Julai, 2025 Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Ndg. Methuthela Stephen Ntonda kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 15 Agosti, 2024.
Meneja Usajili na Kumbukumbu kutoka Ofisi ya Hakimiliki Tanzania (COSOTA) Bw. Philemon Kilaka akitoa mafunzo ya hakimiliki na umuhimu wa usajili wa kazi za Sanaa na Uandishi kwa Wasanii na Waandishi wa vitabu wa Songea Mjini leo tarehe 27.04.2024. katika semina ya mafunzo kwa wadau hao iliyoandaliwa na taasisi zilizochini ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo zinazosimamia kazi za Sanaa nchini.
Muwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu Shirika la Miliki Bunifu la Kikanda la Afrika (ARIPO) Amadu Bah (kulia) akikanidhi hundi ya mfano ya mgao wa mirabaha wa msanii Raymond Mwakyusa (Rayvanny) iliyopokelewa kwa niaba yake na Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki na mdau wa muziki Mhe. Shaban Hamis Taletale, katika hafla ya mgao wa mirabaha, Julai 21, 2023 Jijini Dar es Salaam.
Kamishna wa Bima TIRA Dkt. Baghayo Saqwera (kushoto) akikabidhi hundi ya mfano ya mgao wa mirabaha wa msanii Nasibu Abdul (Diamondplatinumz) iliyopokelewa kwa niaba yake na Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki na Mdau wa muziki Mhe. Shaban Hamis Taletale, katika hafla ya mgao wa mirabaha, Julai 21, 2023 Jijini Dar es Salaam.
Msanii wa Muziki wa Singeli nchini Sholo Mwamba akiwa ametembelea Ofisi ya Hakimiliki Tanzania iliyopo Banda la Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kupata elimu ya hakimiliki na usajili wa kazi Juni 30, 2023 Jijini Dar es Salaam katika Maonesho ya Biashara ya Sabasaba
Mheshimiwa Salma Kikwete Mbunge wa Jimbo la Mchinga na Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa ametembelea banda la Ofisi ya Hakimiliki Tanzania - COSOTA Juni 06, 2023 kupata elimu ya Hakimiliki katika Maonesho ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo yanayoendelea katika Uwanja wa Bungeni Jijini Dodoma.
Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Ally Kiba (kushoto) akipokea hundi ya mfano wa mgao wake wa mirabaha katika mgao wa mirabaha uliyotangazwa tarehe 28 Januari, 2022.