Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Balozi Dkt. Pindi Chana (kulia) akimkabidhi jarida la hakimiliki Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo (kulia) mara baada ya uzinduzi wa jarida hilo uliyofanyika Jijini Dodoma Mei 18,2023 katika semina ya mafunzo ya hakimiliki kwa wabunge wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria ndogo na katikati ni Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo Prof. Kitila Mkumbo.
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) (katikati) akizindua Jarida la Hakimiliki la Ofisi ya Hakimiliki (COSOTA) mara baada Semina ya Wabunge wa Kamati ya Elimu, Utamaduni na Michezo pamoja na Kamati ya Kudumu ya Bunge Sheria Ndogo kuhusu Hakimiliki na mabadiliko ya Sheria na Kanuni mpya iliyofanyika Mei 18, 2023 Jijini Dodoma.
Mbunifu wa Mfumo wa Sheria Kiganjani Wakili Neema Magimba akipokea tuzo ya ubunifu huo katika kipengele cha Kazi zinazolindwa na Sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki zilizosaidia jamii kwa kiasi kikubwa, kutoka kwa Katibu Mkuu Wizara ya Uwekezaji, Biashara na Viwanda Dkt.Hashil Abdallah katika siku ya Maadhimisho ya Miliki Bunifu Duniani iliyofanyika tarehe Aprili 28,2023 Jijini Dar es Salaam.
Msanii wa Filamu kutoka Tamthilia ya Juakali Hellen maarufu kama Love akipokea tuzo kwa niaba ya Mtayarishaji wa Tamthilia ya Jua kali Leah Mwendamseke maarufu kama Lamatah kwa Kipengele cha Kazi zinazolindwa na Sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki iliyowanufaisha wadau wengi, katika siku ya Maadhimisho ya Miliki Bunifu Duniani iliyofanyika tarehe Aprili 28,2023 Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan akimwapisha Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Hamis Mohamed Mwinjuma (Mb) katika Ikulu ya Jijini Dodoma Februari 2023.
Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Ally Kiba (kushoto) akipokea hundi ya mfano wa mgao wake wa mirabaha katika mgao wa mirabaha uliyotangazwa tarehe 28 Januari, 2022.
Afisa Mtendaji Mkuu na Msimamizi wa Hakimiliki Doreen Anthony Sinare akiwa katika picha ya pamoja na Mtaalam wa Mifumo ya Udukuzi na Miliki Bunifu na Mshauri wa Sheria kutoka Idara ya Haki nchini Marekani Tanya Hill (wapili kushoto) akiwa amembatana na Afisa wa Ubalozi wa Marekani Tanzania Jeremy Beck, mara baada ya mazungumzo yaliyofanyika katika Makao Makuu ya Ofisi ya Hakimiliki Tanzania, Novemba 30, 2022.
Naibu Waziri Wizara ya Utamduni, Sanaa na Michezo Mhe.Hamis Mwinjuma (Mb) (aliyeketi katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa wa COSOTA alipowatembelea baada ya kuapishwa kwake.
Majaji kutoka Mahakama Kuu mbalimbali nchi wakiwa katika picha ya pamoja baada ya ufunguzi wa Mafunzo ya Hakimiliki kwa Mahakimu yaliyoratibiwa na Chuo cha Mahakama & COSOTA Mkoani Morogoro.
Afisa Sheria COSOTA akitoa Semina ya kanuni uendeshaji wa makampuni ya kukusanya mirabaha (cmo) na kanuni ya 'blanktape levy' kwa kamati mbili za bunge septemba 20,2022 Jijini Dodoma